Juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa umakini mkuu wa idara ya utalii katika hifadhi ya mlima Kilimanjaro Eva Mallya |
Na Dixon Busagaga wa Globu
ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
HIFADHI ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro ,imetoa fursa kwa wananchi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa jumla kupanda mlima Kilimanjaro hadi kilele cha Shira (Shira Plateu) kwa nusu bei yaani shilingi 5,000 kwa watu wazima kuanzia miaka 16 na kuendelea na Shilingi 1,000 kwa watoto kuanzia miaka 5 hadi 15.
Gharama hii ni nusu ya bei halisi ambayo ni shilingi 10,000 kwa watu wazima na 2,000 kwa watoto.Ofa hii inaanza Mei 15 hadi Mei 18 mwaka huu,Safari hiyo itakuwa ya kutwa nzima kwenda na kurudi siku hiyo hiyo na usafiri utatolewa bure na hifadhi (KINAPA).
Vituo vya kujiandikishia ni mgahawa wa Fresh coach Moshi mjini ,Hosptal ya KCMC,Njia Panda ya Himo (Stand ya Same),Bomang’ombe (Kiwire Supermarket) na KINAPA Marangu(Mapokezi).Kazi ya uandikishaji imeanza tayari.Vituo vitakuwa wazi kuanzia saa 2 asubuhi.Wanaopenda kupanda wanashauriwa kufika katika maeneo hayo tajwa.
Vituo vya kuanzia safari ni viwili Mgahawa wa Fresh Coach Moshi mjini na Bomang’ombe (Kiwire Supermarket),Safari itaanza saa moja kamili asubuhi.
Nadhani ni mpango mzuri japo ungehitaji kuongeza muda angalau wa Juma moja. Pia usajili kwa Watu walio mbali ungefanywa kwa Njia ya Ki-electroniki na malipo kadharika ili kuongeza idadi ya watalii wa ndani
ReplyDelete