Na John Gagarini, Kibaha 

 JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia dereva Frank Chabayanga (39) mkazi wa Morogoro wa basi la kampuni ya BM kwa tuhuma za kumgonga mtembea kwa miguu na kusababisha kifo chake. 
 Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei  (pichani) amesema kuwa tukio hilo limetokea Mei 20 mwaka huu majira ya saa 3:30 Usiku eneo la Kwa Mbonde wilayani Kibaha katika barabara kuu ya Dar es Salaam Morogoro. 
 Kamanda Matei amesema kuwa mtuhumiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Yu Tong lenye namba za usajili T 919 CAB alimgonga mtu ambaye jina lake halikuweza kutambuliwa mara moja. Aidha alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo wa kasi ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa kwnye hospitali ya Rufaa ya Tumbi. 
 Kwenye tukio lingine dereva Issa Kidito (64) mkazi wa Dar es salaam anashikiliwa kwa tuhuma za kumgonga mpanda baiskeli na kusababisha kifo. 
 Kamanda Matei amesema kuwa mtuhumiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Land Cruiser hard top lenye namba za usajili namba T 722 ABA aliwagonga wapanda baiskeli na kusababisha kifo cha Mwalimu Hamisi Mtanga (58). 
 Amebainisha kuwa tukio hilo lilitokea kitongoji cha Londondo Kijiji cha Kiwanga Kata ya Chumbi tarafa ya Muhoro wilaya ya Rufiji ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akielekea mkoani Lindi aliacha barabara na kumgonga mwendesha baiskeli huyo ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Mihilu na kufariki papo hapo huku abiria wake Mussa Ndolela akijeruhiwa na kulazwa kituo cha afya Muhoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...