Na Father Kidevu Blog

SHINDANO la Miss Dar City Center limezinduliwa rasmi jana na linatarajiwa kufanyika mei 24 kwaka huu katika ukumbi ambao utatangazwa baade, huku likishirikisha warembo 15.

Akizungumza katika uzinduzi huo jana, mratibu wa shindano hilo, Judith Charles alisema kuwa, mwaka huu shindano hilo litambapwa na vionjo tofauti tofauti ili kulifanya kuwa la aina yake.

Judith alisema kwamba, wameangalia changamoto zilizotokea kwa waandaaji wa waliopita wa shindano hilo, ili kuweza kulifanya kuwa na ubora wa hali ya juu zaidi kuliko ilivyowahi kutokea.

“Tumetumia changamoto ya waandaaji waliopita wa shindano hili na sisi tumeamua kuliboresha zaidi na hivyo tunaamini kabisa kwamba litakuwa katika kiwango cha juu zaidi tofauti na uilivyokuwa hapo mwanzo,” alisema Judith.

Aidha aliongeza kusema kwamba, ana aimani kubwa kwamba Miss Dar City Center ndiko atakakotokea Miss Tanzania 2014, kwani wamejiandaa kwa ukamilifu wa hali ya juu.

Judith alisema kwamba ana imani kubwa na matron ambaye pia ndie mwalimu wa warembo wa shindano hilo, Eshe Rashid kuwa atawapa mafunzo mazuri zaidi yatakayowezesha kuwa bora zaidi jukwaani.

Pia aliongeza kusema kwamba, zawadi kwa washindi wa shindano hilo zitakuwa zimeboreshwa zaidi na hivyo ana imani zitavutiwa zaidi na warembo hao.

Aidha Judith alisema, shindano hilo kwa kiasi kikubwa linafadhiliwa na  Prima, Zanzi, Sky light band, Clouds FM, Dimond Bureu De Change LTD, gazeti la Jambo leo, Klabu Maisha ambako warembo wanafanyia mazoezi, blog ya Wananchi, blog ya Father Kidevu, Michuzi Media Group, Hoteli ya JB Belmont na Machapta Production

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...