Asia Hamisi akiwa amezirai mahakamani
baada ya kuhukumiwa miaka mitano jela

Watu wawili wa familia moja Frank Charles na mkewe Asia Khamis wamehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela au kulipa faini ya shilingi milioni moja kila mmoja kwa kosa la kukutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi.
Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Mbeya Maria Batulaine amewatia hatiani wanandoa hao baada ya  kuridhishwa na ushahidi usio shaka wa mashahidi wanne wa upande wa mashitaka.
Imedaiwa na Mwendesha mashitaka wa Serikali Juliana William amesema kuwa washitakiwa hao walikutwa na kete 100 za bangi Novemba 19 mwaka jana eneo la Makunguru Jijini Mbeya baada ya upekuzi wa Polisi.
Baada ya kusikiliza pande zote mbili aliwapa washitakiwa nafasi ya kujitetea ambapo walisema kuwa wana watoto wawili mmoja akiwa darasa la nne na mwingine akiwa kidato cha tatu hivyo kuiomba mahakama kuwaangalia kwa jicho la huruma kwa kuwa hilo ni kosa lao la kwanza.
Wakati Hakimu Batulaine akitafakari adhabu kwa washitakiwa hao mshitakia wa pili Asia Khamis alianguka ghafla kizimbani na kuzirai na kumwacha Hakimu akiwa kimya kwa muda kabla ya kutoa hukumu.
Mwendesha mashitaka Juliana William aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia ya kuvuta na kuuza madawa ya kulevya.
Hakimu Maria Batulaine aliwahukumu kwenda jela miaka mitano jela au kulipa faini ya shilingi milioni moja kila mmoja na mshitakiwa wa kwanza alikuwa akihaha kutafuta fedha hizo na baadhi ya wasamaria walikuwa wakitoa huduma kwa mkewe baada ya kudondoka kizimbani na  kuzirai.
Na Mbeya yetu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2014

    Mbona miaka mitano ni mingi sana bangi tu au kuna lingine......

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2014

    watu wanakamatwa na madawa ya kulevya kila siku na hatujaona waliofungwa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 07, 2014

    Madawa ya kulevya ni mabaya yanaharibu akili za watu na kusumbua familia nyingi nchini, kabla hujasema hukumu hii ni ndogo fikiria gharama ya kuwa na mtu aliyeathirika na madawa ya kulevya

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 07, 2014

    Aaaaaaah jamani yaani bangi tu mtu anakwenda jela miaka 5? Mbona huku kwetu Njombe ni mboga? Mbegu zake tunatengeneza mafuta ya kula? Mbona hatujawehuka?

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 08, 2014

    Unaanguka chini na kuzirai?

    Mbona ulivyokuwa unawapandisha Kichaa vijana kwa kuwauzia Bangi hukuanguka kwa masikitiko?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...