Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (PE. 1656) akila kiapo rasmi mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Rukwa Msomi Enock Kasian Matembele kwa mujibu wa sheria ya usajili wa wahandisi (Engineer's Registration Act (Cap 63), Kanuni na sheria ndogo zote zilizowekwa na zitakazowekwa ikiwemo mwendo wa utendaji kazi pamoja na maadili katika taaluma ya uhandisi. 

Kiapo hicho kimeafanyika leo katika ukumbi wa "video comference" uliopo katika jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo leo tarehe 23-05-2014. Awali kiapo hicho kilikuwa kifanyike Dodoma pamoja na mawaziri na wabunge wengine ambao ni wahandisi lakini kutokana na majukumu yasiyozuilika Eng. Manyanya ameruhusiwa aape akiwa Sumbawanga.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Rukwa Msomi Enock Kasian Matembele wakisaini hati ya kiapo hicho mbele ya mashuhuda mbalimbali walioalikwa katika hafla hiyo fupi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akizungumza muda mfupi baada ya kuapishwa, pamoja na mambo mengine amesema ni marufuku kwa wahandisi ambao hawajasajiliwa kuidhinisha au kupitisha  kazi za miradi mikubwa katika Mkoa wake wa Rukwa. Aliendelea kusema kuwa kwa Mhandisi yeyote ambaye hajasajiliwa hana mamlaka ya kutumia tittle PE. Eng.....kama inavyoelekezwa kwa mujibu wa sheria, hata hivyo aliwaahidi wahindisi wote ambao hawajasajiliwa katika Mkoa wa Rukwa ushirikiano katika kuwapa miongozo itakayowawezesha kukamilisha taratibu zao za usajili. Kwa upande mwinine aliipongeza bodi ya ERB kwa kuwa madhubuti na kuweka utaratibu unaowezesha uwajibikaji. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...