Kila Tar 18 Mei Jamii husherekea siku ya Makumbusho Duniani, hapa Tanzania sherehe hizi Kitaifa zitafanyika Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar Es Salaam. Katika siku hii muhimu, Makumbusho ya Taifa inatarajia kuufungua rasmi Ukumbi wa Maonesho ya kudumu ya Sanaa.

Kutokana na umuhimu wa siku hii Makumbusho ya Taifa inawakaribisha Watanzania wote kutembelea Makumbusho ya Taifa ili kujifunza mambo mbali mbali kupitia vitu na naarifa zinazothaminiwa na jamii zilizo hifadhiwa na Makumbusho.

Ufunguzi unatarajiwa kuanza saa 10 :00 jioni na  utapambwa na Kikundi cha Sanaa cha GODYKAOZYA & THE TONGWA ENSEMBLE kutoka Bagamoyo.

Kuanzia Tar 16 - 18  watu wote watapatiwa huduma za Kimakumbusho BURE.
Usikose fursa hii Muhimu kwa ongezeko la uelewa wako juu ya nchi yako.

Makumbusho ya Taifa  na Nyumba ya Utamaduni ipo Posta mtaa wa Shaaban Robert mkabala na chuo cha usimamizi wa Fedha(IFM)

Karibuni sana.
SIXMUND J. BEGASHE

MRATIBU WA MAANDALIZI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...