Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhi hundi ya jumla ya Shilingi Milioni miamoja na Hamsini 150m/- kwa wawakilishi wa kituo cha kulea watoto yatima cha Moyo wa Huruma kilichopo mkoa wa Geita.
Fedha hizo si sehemu ya shilingi milioni mia saba(700m/-) alizokabidhi Rais Kikwete jana usiku kwa taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya ukimwi Tanzania.Fedha hizo zinatokana na kampeni ya kukusanya fedha kwa njia ya kupanda mlima Kilimanjaro kila mwaka ambapo wafadhili mbalimbali huchangia watoto na watu wengine.Pichani watoto wawili watakaopanda mlima
Kilimanjaro Jacob Musa(watatu kushoto) na Julitha Sylvester(wapili kulia) wanaofadhiliwa na kituo cha Moyo wa huruma wakipokea hundi ya kituo chao.
Wengine katika picha kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dr.Florence Turuka,Mkurugenzi Mkuu wa TACAIDS Bi Fatma Mrisho,Mkurugenzi Mtendaji wa Geita Gold Mines Bwana Michael Van Anen(watano kushoto),Naibu Waziri wa Afya Dr.Steven Kebwe, na kulia ni msimamizi wa kituo cha kulelea watot yatima cha Moyo wa Huruma Sista Adalbera Mukure.
Katika hafla ya jana ya kuchangia kampeni hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam zaidi ya shilingi milioni mia tisa 900m/- zilikusanywa(picha na Freddy Maro)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...