ABUJA, Nigeria, May 8, 2014/ -- Rasilimali za Afrika zenye utajiri mwingi zinatoa nafasi ya kipekee ya ufanisi katika uimarishaji wa maisha ya raia wa Afrika, yasema ripoti mpya kubwa iliyozinduliwa leo na Kofi Annan, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, lakini mara nyingi sana rasilimali hizi huporwa na maafisa wafisadi pamoja na wawekezaji wa kigeni. Aidha, Ripoti hii inaonyesha kwamba kuongezeka kwa ukosefu wa usawa vilevile kunaizuia Afrika isiikamate nafasi hii ya maendeleo.

Ripoti hii ya 2014 ya Jopo la Maendeleo ya Afrika (http://www.africaprogresspanel.org), Nafaka, Samaki, Pesa: Kugharamia mageuzi ya Kijani kibichi na Samawati, inawahimiza viongozi wa kisiasa wa Afrika kuchukua hatua hususa sasa ili kupunguza ukosefu wa usawa kwa kuwekeza katika kilimo. Pia, inataka hatua ya kimataifa kuchukuliwa ili kukomesha kile kinachotajwa kuwa uporaji wa sekta za mbao na uvuvi.

“Baada ya zaidi ya mwongo mmoja wa ukuzi, kuna mengi ya kushangilia,” Bwana Annan atawaambia viongozi wa kisiasa na wa kibiashara, wakati wa kuzinduliwa kwa ripoti hii katika mkutano wa Baraza la Kiuchumi la Ulimwengu kwa Afrika (World Economic Forum for Africa). “Lakini ni wakati wa kuuliza kwa nini ukuzi mkubwa wa jinsi hii haujasaidia hata kidogo kuwainua watu kutoka katika umasikini na kwa nini utajiri mwingi wa Afrika umeharibiwa kupitia mazoea ya ufisadi na uwekezaji usio mnyoofu.”#

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...