ABUJA,
Nigeria, May 8, 2014/ -- Rasilimali za Afrika zenye utajiri mwingi
zinatoa nafasi ya kipekee ya ufanisi katika uimarishaji wa maisha ya
raia wa Afrika, yasema ripoti mpya kubwa iliyozinduliwa leo na Kofi
Annan, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, lakini mara nyingi
sana rasilimali hizi huporwa na maafisa wafisadi pamoja na wawekezaji wa
kigeni. Aidha, Ripoti hii inaonyesha kwamba kuongezeka kwa ukosefu wa
usawa vilevile kunaizuia Afrika isiikamate nafasi hii ya maendeleo.
Ripoti hii ya 2014 ya Jopo la Maendeleo ya Afrika (http://www.africaprogresspanel.org),
Nafaka, Samaki, Pesa: Kugharamia mageuzi ya Kijani kibichi na Samawati,
inawahimiza viongozi wa kisiasa wa Afrika kuchukua hatua hususa sasa
ili kupunguza ukosefu wa usawa kwa kuwekeza katika kilimo. Pia, inataka
hatua ya kimataifa kuchukuliwa ili kukomesha kile kinachotajwa kuwa
uporaji wa sekta za mbao na uvuvi.
“Baada
ya zaidi ya mwongo mmoja wa ukuzi, kuna mengi ya kushangilia,” Bwana
Annan atawaambia viongozi wa kisiasa na wa kibiashara, wakati wa
kuzinduliwa kwa ripoti hii katika mkutano wa Baraza la Kiuchumi la
Ulimwengu kwa Afrika (World Economic Forum for Africa). “Lakini ni
wakati wa kuuliza kwa nini ukuzi mkubwa wa jinsi hii haujasaidia hata
kidogo kuwainua watu kutoka katika umasikini na kwa nini utajiri mwingi
wa Afrika umeharibiwa kupitia mazoea ya ufisadi na uwekezaji usio
mnyoofu.”#
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...