WANAHABARI mkoa wa Wa Lindi wakiongozwa na Mwenyekiti wao Bw Abdulaziz Ahmeid wameadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani kwa kutoa msaada kwa jamiii baada ya kutoa msaada wa Vifaa mbalimbali katika wodi za wazazi na watoto katika Hospital ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi
Wanahabari hapo pia walipimwa afya zao na  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani humo ili kila mmoja afanye kazi zake huku akijua Afya yake 
 Akiongea baada ya hafla hizo Bw. Abdulaziz Ahmeid alieleza kuwa katika maadhimisho hayo ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Arusha ambayo yana kauli mbiu ya Uhuru wa Habari kwa maendeleo na utawala bora Ambapo wanahabari wameamua kurudi kwa jamii kwa kuona umuhimu wa kusaidia wagonjwa,Wazee na Walemavu 
"Ni Vyema waandishi tukajenga Utayari wa kusaidia Jamii na ndizo zenye Uhitaji wa misaada muhimu na hata kihabari kuliko kujikita na wanasiasa kwa maslahi yao na wakati wao tu Muhimu Tujitambue tutetee haki zetu ikiwemo Kuajiriwa na kufungwa kwa mikataba kuliko ilivyo sasa zaidi ya asilimia 90 HATUJIELEWI.
"Sambamba na hilo Tujikite katika kuandika habari za Uchunguzi na fursa zipo kupitia TMF..Alimalizia Abdulaziz.
Nae Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Lindi Bi Fortunata Kullaya ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika sherehe hizo zilizokutanisha waandishi toka wilaya zote za mkoa wa Lindi aliwataka Waandishi kuandika habari kwa kufuata maadili ili wasijiingize katika matatizo hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa katiba na kuelekea katika uchaguzi mkuu hapo mwakani kwa kuwa wanahabari ni watu muhimu katika jamii.
Pia aliwataka kufika vijijini kubaini baadhi ya changamoto ambapo pia aliwahakikishia kuwa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF sasa ndio mkombozi wa huduma za afya hivyo pelekeni Ujumbe Jamii Ijiunge na ipate Tiba kwa Unafuu zaidi Nyie ni wadau wakubwa wa NHIF, hivyo mbaini kuwa kalamu zenu zinaweza kujenga au kubomoa hivyo bima ya afya Tawi Lindi 
"Tumeona ni siku muhimu sana kujumuika pamoja kwa kuwapima afya zenu ili mfanye kazi mkijijua Aidha katika maadhimisho hayo pamoja na lutoa msaada kwa Wagonjwa wa hospital ya Rufaa ya Sokoine na kupimwa kwa Afya za Waandishi 
hayo yalifuatiwa na Tafrija Fupi ya Kutakiana heri iliyojumuisha waandishi na Wenza wao pamoja na wadau wengine wa habari iliyofanyika katika Fukwe za Santorin Beach Manispaa ya Lindi
 Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa Habari Lindi Bw. Abdulaziz Ahmeid akipimwa afya yake na daktari wa NHIF Timoth Mwasajone katika kuadhimisha siku ya Uhuru wa Habari
 Picha ya pamoja ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa Mfuko wa NHIF Mara baada ya mfuko huo kujitolea kupima Afya za waandishi wa Lindi
  Mwandishi wa Tbc Lindi Martina Ngulumbi akimbeba  mtoto toka kwa mama alietoka kujifungua siku ya uhuru wa habari
 .Mwenyekiti wa LPC ,Abdulaziz Ahmeid akikabidhi msaada Kwa Muuguzi wa zamu Bi Habiba Chitanda msaada uliotolewa na Wanahabari wa Lindi
Mwenyekiti Abdulaziz akisalimia baadhi ya watoto waliolazwa katika wodi ya watoto katika hospitali ya Sokoine mjini Lindi mara baada ya kukabidhi vifaa mbalimbali katika kusaidia jamii katika siku ya uhuru wa habari

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...