WANANCHI wa Kata ya Tembela Wilaya ya Mbeya Vijijini wameiomba Serikali kusaidia kukiwezesha Kituo cha Afya Simambwe ili kifanye kazi saa 24 ili kuwasaidia muda wote wananchi wanaohudumiwa na kituo hicho hasa wajawazito.

Kauli za ombi hilo zimetolewa hivi karibuni kwa nyakati tofauti na wananchi hao walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi katika vijiji vyao alipowatembelea kuangalia changamoto anuai za huduma za kijamii vijijini Kata ya Tembela.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Ilembo Usafwa, Richard Ngomela alisema licha ya kijiji hicho kuwa takribani umbali wa kilometa tatu na nusu kukifikia kituo cha afya Simambwe wanakitegemea hivyo kuomba wahudumu kufanya kazi saa 24 ili wapate huduma muda wote.

Alisema kitendo cha kituo hicho kufanya kazi mchana pekee kimekuwa kikishindwa kuwasaidia wagonjwa wa usiku na hasa wajawazito jambo ambao limewafanya baadhi yao kuangaika nyakati za husiku kihuduma na wengine kujifungulia nyumbani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...