Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Samuel Sitta anatarajia kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara  kwa mwaka wa Fedha 2014/2015 kesho tarehe 22 Mei, 2014, ambapo atazungumzia utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2013/2014 na makadirio ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
Hotuba hiyo itapatikana kwenye tovuti ya Wizara www.meac.go.tz na kwenye vyombo mbalimbali vya habari mara baada ya Mhe. Waziri kumaliza kuisoma Bungeni.
Tunawakaribisha wadau mbalimbali wa masuala ya Mtangamano wa Afrika Mashariki na wananchi kwa ujumla kufuatilia kwa karibu hotuba hiyo ili kuongeza uelewa wa masuala ya Matangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Imetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki
+255 222126827, 2126830
+255 713341354
Email: ps@meac.go.tz
Website: www.meac.go.tz

21 Mei, 2014

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...