Na Woinde Shizza, Arusha 
Jaji mstaafu Mark Bomani leo amezindua rasmi video ya wimbo wa waandishi wa habari ujulikanayo kwa jina la Uhuru wangu pamoja na albamu mpya ya msanii wa mziki wa nyimbo za asili Mrisho Mpoto ijulikanayo kwa jina la Waite katika kilele cha maathimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani jijini Arusha. 
Uhuru wangu uko wapi mwanahabari mie,kalamu yangu,sauti yangu kamera yangu leo ndio kaburi langu mie Huo ndio wimbo wa kundi la Mrisho Mpoto Band ambalo ulikuwa ukiwaburudisha wanahabari katika uzinduzi wa albamu Mrisho Mpoto Band,unaoelezea mambo mbalimbali wanayokumbana nayo wanahabari wa vyombo mbalimbali vya habari. 
Akighani mashairi ya wimbo huo katika uzinduzialisema poleni sana misa Tanzania,TMF,MOAT,UTPC ,TCRA kama mtu ile timu ya watu watano tuyioituma Ujerumani ,Norway,Sweden ipo wapi ripoti yake 
kiongea wakati wa uzinduzi wa albamu hiyo pamoja na wimbo huo wa wanahabari msanii mrisho mpoto alisema kuwa yeye alifarijika sana pale alivyofatwa na wanahabari na kumuomba awatungie wimbo ambao unawahusu wanahabari pamoja mambo ambayo yanawakabili. 
 Alisema kuwa wamekaa wakashauriana na timu yake na bendi yake kuwa watu wasanii wengi wamekuwa wakizindua albamu kwa kuweka viingilio vikubwa kualika watu wengi lakini yeye binafsi ameamua kuzindua albamu hii katika siku hii ya waandishi wa habari kwa kuwa wamemtoa mbali na ana kitu cha kuwapa zaidi ya kuwapa zawadi hii ya kuzindua albamu yake mbele yao. Alibainisha kuwa mbali nakuzindua albamu hiyo pia kwa kuwa waandishi wamempa hadhi ya kuwatungia wimbo pia anajitolea kuweka wimbo huu wa waandishi wa habari ndani ya albamu yake ili kila mtanzania na mshabiki wake ambaye atanunua albamu yake aukute wimbo ndani ya albamu yake. 
"Hii albamu yangu itakuwa na nyimbo zangu zote ikiwa na wimbo wa nikipata nauli adi nyimbo zake zote ambazo zinajulikana na kiukweli najisikia kulia sana kupewa heshima hii nzito ya kuzindua albamu yangu na ata jana nilivyokuwa nakuja uku nilikuwa na zunguma na mh bomani kuwa hii kwangu itakuwa ni historia katika maisha yake"alisema mpoto 
Katika wakati wimbo huu ukiendelea wanahabari walionekana wakitoa machozi kwa kuuzunishwa na tenzi zilizopo katika wimbo huu kwani msanii huu ameuimba kiualisiazaidi.

Jaji mstaafu Mark Bomani akiongea wakati wa kuzindua rasmi video ya wimbo wa waandishi wa habari ujulikanayo kwa jina la Uhuru wangu pamoja na albamu mpya ya msanii wa mziki wa nyimbo za asili Mrisho Mpoto ijulikanayo kwa jina la Waite katika kilele cha maathimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani jijini Arusha. 
Jaji mstaafu Mark Bomani akizindua rasmi video ya wimbo wa waandishi wa habari ujulikanayo kwa jina la Uhuru wangu pamoja na albamu mpya ya msanii wa mziki wa nyimbo za asili Mrisho Mpoto ijulikanayo kwa jina la Waite katika kilele cha maathimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani jijini Arusha. Chini Mrisho Mpoto akielezea wimbo wake.
Picha na Woinde Shizza wa Globu ya Jamii, Arusha

Video na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii, Moshi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...