NA  HAPPINESS MNALE

KWA mara ya kwanza  kwenye ukumbi wa Maisha Plus (Pilice Mess) kutafanyika tukio la aina yake la kumsaka Redds Miss Pwani 2014 usiku wa leo.

Katika Shindano hilo ambalo  litakuwa ndiyo sehemu ya kuuzinduz ukumbi huo ambao leo  hii ndiko  kutakuwa na burudani kubwa ya muziki wa dansi kutoka katika  bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Next level’ wakiongozwa na  mzawa wa mkoa wa Pwani  Ally Choki almaarufu kama ‘Mwarabu wa Kibaha’ ambao nao wameahidi kutoa burudani ya kihistoria kwenye onyesho hilo.

Bendi hiyo ambayo inatamba na vibao vingi ambvavyo vimeipa sika kama ‘Regina’ na nyinginezo.Mbali ya Choki ambaye atakuwa na kikosi chake kikali cha wacheza shoo kinachoongozwa na Mussa Hassan Nyamwela pamoja na wanenguaji wa kike kama Maria Soloma , Asha Said ‘Sharapova’ , Otilia na wengineo watanogesha na kuacha historia siku hiyo .

Katika shindano hilo jumla ya warembo Kumi watapanda jukwaani ambao  Khadija Sihaba, Glory  Jige,  Irene Rajab, Mary Samwel, Arafa Shabani, Jeniffer David, Judea Joseph, Mary Mpelo,Roksana Msangi  na Faith.

Mshindi wa  Miss  Pwani ndiye atapata nafasi ya kuuwakilisha Mkoa huo  katika  shindano la kanda ya Mashariki na baadaye katika fainali za Redd’s Miss Tanzania 2014.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...