Tarehe kama ya leo ya maka 2013 mpendwa wetu Anna Ntamubano Gwitaba uliitwa na Bwana maana yeye alikupenda zaidi na tayari amekuandalia taji zuri kwa ajili ya Ufalme wake .
Wewe ulikuwa moja ya maua mazuri yaliyopandwa katika bustani ya Bwana na wakati ulipochanua na kuvutia Bwana alikuchuma na kukuweka mahali pazuri mno.
Daima unakumbukwa na familia yako wakiwemo watoto wako (Adam, Irene, Edgar na Kelvin) na baba yao, mama yako mpendwa (Bibi Naomi), dada zako, kaka zako, watoto wote uliowalea, wajukuu, mawifi, mashemeji, wajomba, mashangazi, wakwe, marafiki, wafanyakazi wenzako na majirani wote.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa,
Jina lake lihimidiwe
AMINA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...