MAREHEMU MWASHABAN A. LIGANJA

Mpendwa Mama,
Mama unatimiza miaka saba (7) sasa toka ututangulia mbele ya haki. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa muda wote uliokuwa nasi. Si tu kuwa Mama bali pia kuwa mtu wa pekee miongoni mwetu Mama. Ulibarikiwa mambo mengi ambayo tukianza kuyaorodhesha hapa tunaweza kujaza kitabu ila kwa ufupi UPENDO usiokuwa na kipimo.

Mama DAIMA utakumbukwa na Mumeo Mpendwa George Mapango, wanao Mariam (Chuma), Eva (Hawa), Jackson (Kibabu), Patrick (Said), Richard na watoto wote kwa upande wa Dada zako na kaka zako. Mkweo Deogratius Sakawa, Wajukuu zako Precious (P), Pricilla na Jasmine. Wadogo zako, Ndugu, Jamaa, Marafiki zako, Majirani na Wafanyakazi Wenzako.
Tutaendelea kufuata ushauri wako na mema mengi uliyotufundisha. Kwa upendo wako unatuunganisha familia na tutaendelea kukumbuka busara zako na hekima daima. 
KISOMO KITAFANYIKA LEO  TAREHE
 07 JUNI, 2014 SAA 04.00 ASUBUHI.

INNA LILAH WAINA LILAH RAJIUUN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2014

    Mafundisho yako tutayaishi milele. Juzi nilisoma diary yako nikahisi nimeongea na wewe. Niliisikia sauti yako moyoni mwangu,Mama.
    Daima tutakukumbuka huku tukiwa na tumaini la kuwa siku moja kuonana nawe. We will always cherish good memories and time we shared together.
    R.I.P Mama.
    Mariam Chuma (Dachu).

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...