Leo hii Ijumaa Juni 20, 2014, kuanzia saa 5 mchana kwa saa za Marekani na saa 12 jioni kwa saa za Tanzania nimegundua kwamba akaunti yangu binafsi ya barua pepe kidundo2001@yahoo.com imevamiwa na wahalifu. 
Nimechukuwa hatua stahili na za haraka katika kushughulikia tatizo hili. Naomba kuwashukuru wote walionitanabahisha kwa kufahamu kwamba niko Washington DC, Marekani,  na wakashangazwa kupokea barua pepe nyingi ambazo zimedai kwamba niko Nassau, Bahamas, Manila Philippines, Rio de Janeiro, Brazil na Singapore na kwamba nimepata matatizo ya kuvamiwa na majambazi na kuibiwa kila kitu na hivyo kuomba msaada wa dharura.
   Naomba kuchukuwa fursa kutoa taarifa hii  kwamba mimi niko salama Washington DC, Marekani, na ninaendelea na shughuli zangu za kazi katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ya matatizo yeyote. Pia naomba mtu yeyote atayepata email kwa anuani hiyo aipuuze, si ya kweli. Nitatoa tena taarifa mara nitapokuwa na anuani yangu halisi muda si mrefu ujao.
   Namshukuru Ankal Muhidin Issa Michuzi kwa kunitumia taarifa ya kwanza kuhusiana na uhalifu huu, na kunishauri kuchukua hatua haraka.

Suleiman Saleh
Washington DC

Juni 20, 2014

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 21, 2014

    haya matatizo hujitokeza sana kwa accounts za hotmail na yahoo

    jaribu kutumia gmail zaidi pamoja na kuweka password ngumu yenye numbers na herufi kubwa na ndogo ukiweza

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...