![]() |
Wachezaji wa Spain wakitoka nje ya uwanja baada ya kuvuliwa ubingwa wa dunia na kufungashiwa virago na Chile (chini) |
Na Sultani Kipingo
Usiku wa kuamkia leo ulikuwa wa aina yake huko Brazil. Utawala wa Wafalme
wa Kombe la Dunia, Spain, uliota mbawa. Mchezaji wa Australia alifunga goli la
mwaka, na Mfalme Willem-Alexander na Malkia Maxima wa Uholanzi walisisimkwa mno
kuona nchi wanayoongoza ikipiga hatua mbele kuelekea Ubingwa kiasi hata
wakapozi picha za selfie na Arjen
Robben, Robin van Persie na wenzao kwenye chumba cha kuvalia.
Siku ya saba ya michuano hii ilainzia mji wa Porto Alegre.
Ikaishia takriban maili 2000 kutoka hapo (naam, Brazil kubwa ati), Ambapo
Uholanzi na Chile wakapata tiketi kuingia raundi ya 16 bora na mchezo mkononi.
Hapo Australia, Spain na Cameroon ndio wameshafungashiwa
virago, huko Croatia ikiwa imeshinda vizuri kujiweka katika kinyang’anyiro cha
utatu na Brazil na Mexico kuwania tiketi mbili za kuingilia hatua ya mtoano.

Serikali ya Brazil imeamua kuwatimua mashabiki hao wapatao
85 na kuwapa masaa 72 kuondoka nchini humo kwa kuvamia uwanjani na
kuwaparaganya waandishi wa habari ambao ilibidi watoke mbio kwa tukio hilo la
aina yake katika Kombe la Dunia.
Matokeo:
Australia 2-3 Netherlands
Spain 0-2 Chile
Cameroon 0-4 Croatia
Hivi toka tupate uhuru Tanzania iliwahi kusogelea au kufikia kombe la dunia hata wakati mmoja?
ReplyDeleteHivi toka tupate uhuru Tanzania iliwahi kusogelea au kufikia kombe la dunia hata wakati mmoja?
ReplyDeleteKwani ni lazima?