Katika kuendelea kusherehekea Muungano wetu na pia kujiunga na wenzetu wa nchi ya Zambia ambao nao mwaka huu wanasherehekea miaka 50 tangu wapate Uhuru (25 Oktoba), Ubalozi wa Tanzania nchini Zambia unapenda kuwajulisha kuwa umeandaa maonesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania.

Ubalozi wa Tanzania nchini Zambia unachukua nafasi hii kuwakaribisha rasmi Watanzania kuja kushiriki katika maonesho haya. Tuna amini ni nafasi nzuri ya kujitanganza na kuonana uso kwa uso na wadau mbalimbali ili kupanua wigo wa biashara.
Maonesho haya ambayo yamebeba jina la "TANZANIA WEEK" yatafanyika katika viwanja vya Ofisi ya Ubalozi Lusaka, Zambia, kuanzia tarehe 25 hadi 31 Julai 2014.

Kwa maelezo zaidi na mawasiliano tumia njia zifuatazo:

     Nukushi ya Ubalozi: tanzanhighcom@zambia.co.zm
     Namba ya Simu: +260211253323/4 
     
Maafisa wa Ubalozi;
      
i) Bibi Justa M. Nyange - simu ya kiganjani +260-979-401-433 
      Nukushi : kitutuj@yahoo.com

    ii) Bw. Richard M. Lupembe  - simu ya kiganjani +260-965-031-754
          Nukushi : rlupembe@yahoo.com.

    iii) Bw. Mogosi S. Munatta - simu ya kiganjani +260-979-411-011
          Nukushi : munatta@yahoo.co.in.
      
   iv)  Bw. Huddy A. Kiangi …….simu ya kiganjani +260-977-934-240
         Nukushi : hkiangi@yahoo.com.


KARIBU SANA LUSAKA, ZAMBIA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...