Washiriki wa Nice & Lovely Miss Tanga 2014 jana walitembelea kituo cha matangazo cha redio Mwambao Fm cha jijini Tanga kujionea jinsi kituo hicho kinavyorusha matangazo yake.

Wakiwa katika kituo hicho, warembeo hao walipata fursa ya kuzungumzia shindano hilo huku kila mmoja akitamba kuibuka mshindi siku ya jumamosi ya tarehe 21/06/2014 ndani ya Mkonge Hotel kuanzia saa moja usiku.

Baadaye leo washiriki hao watatembelea kituo cha redio cha Breeze Fm pia cha jijini Tanga na kesho wanataraji kwenda kutoa msaada katika moja ya vituo vya kulea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Shindano hili limedhaminiwa na Nice & Lovely, EATV, Redd's, Tanga Beach Resort, Breeze Fm, CXC Africa, Rweyunga Blog na Mwambao Fm. Malkia wa mipasho Afrika Mashariki, Bi Hadija Omary Kopa ndiye atakayetoa burudani siku hiyo
Washiriki wa Nice & Lovely Miss Tanga 2014 wakiwa wamelizunguka gari ambalo atakabidhiwa mshindi wa kwanza katika shindano hilo.
Washiriki wa Nice & Lovely Miss Tanga 2014 wakiwa wamesimama mbele ya basi lao muda mfupi baada ya kutoka kutembelea kituo cha redio Mwambao Fm jijini Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 18, 2014

    Duhhh Tanga kazi ipo Wasichana wakaliii!

    Sasa Waandaaji mnaonaje mkinipatia mimi Mgosi wa Kaya nipo huku Darisalam namba zao za simu ili nijaribu bahati yangu kutoka kwa mmoja hadi mwingine?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...