Rais wa Shirikia la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Prof. David Grimes  ( wanne kushoto kutoka mstari wa mbele) na Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Michel Jarraud (watatu kutoka kushoto mstari wa mbele) katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati Kuu ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO EC). Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, Dkt Agnes Kijazi (wa kwanza kutoka kushoto waliosimama) akiwa miongoni mwa wajumbe 37 wa kamati hiyo kuu ya WMO.  

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Dkt. Agnes Kijazi akiwa mmoja wa wajumbe wa kamati  kuu ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani anashiriki mkutano wa 66 wa Kamati Kuu ulioanza tarehe 18 Juni 2014 huko Geneva. Mkutano wa mwaka huu utajadili masuala ya hali ya hewa katika maeneo yafuatayo : Upunguzaji wa madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa, Utoaji huduma za hali ya hewa, mpango maalum wa kuhakikisha huduma za hali ya hewa zinawafikia walengwa zikiwa na ubora (Global Framework for Climate Services-GFCS), Mkakati endelevu  wa kujenga uwezo, mfumo wa uangazi wa hali ya hewa wa Shirika la Hali ya Hewa Dunia na shughuli za utafiti. Kwa maelezo zaidi tembelea www.wmo.int   
IMETOLEWA NA: MONICA MUTONI , AFISA UHUSIANO,TMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...