Banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF, lililoko kwenye viwanja vya Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa jijini Dar es Salaam. PPF inashiriki maionyesho ya 38 ya biashara ya mwaka huu 2014 na inawakaribisha wananchi wote kujonea na kupata taarifa ya huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo
 Afisa Michango wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Gloria Maboya, (Kulia), akiwapatia taarifa za michango, wanachama wa PPF, waliotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonyeshjo ya 38 ya biashara ya kimagtaifa kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
 Afisa Michango wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Gloria Maboya, (Kushoto), akitoa elimu kuhusu Mfuko huo, kwa mwanachama huyu aliyetembelea banda la PPF lililoko viwanja vya Maonyesho ya biashara ya kimataifa ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
 Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, (Kushoto), akimkabidhi Mwnanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, taarifa yake ya michango alipotembelea banda ya PPF, kwenye siku ya pili ya Maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam
Mratibu wa Kanda za Mfuko wa Pensheni wa PPF, Mbaruku Magawa (Kushoto), akimfafanulia Mwanachama wa Mfuko huo, kuhusiana na michango yake, alipotembelea banda la PPF, kwenye siku ya pili ya Maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...