DSC_0397
Mkali wa muziki wa reggae nchini, Ras Innocent Nyanyagwa na bendi yake wakitumbuiza kwenye tamasha la 17 la ZIFF 2014 linaloendelea kwenye viunga vya Ngome Kongwe visiwani Zanzibar.

DSC_0438
DSC_0461
Ras Inno akiwapa mzuka mashabiki wake kwa kuruka na wamasai ndani ya Ngome Kongwe alipotoa show ya aina yake baada ya kuhudhuria tamasha la ZIFF miaka minane iliyopita.

MKALI wa muziki wa rege nchini Innocent Nganyagwa anajiandaa kutoa filamu inayohusu maisha yake kama sehemu ya kufunza kizazi kijacho kuhusu muziki huo.
Filamu hiyo ambayo itabeba maisha yake ya kuishi katika muziki wa reggae inatolewa kama ile ya Jimmy Cliff  "The hader they Come".
Ras Nganyagwa mwenye albamu nne na tuzo tano za hapa nyumbani alisema pamoja na kukaa kimya kwa muda mrefu alikuwa hajaondoka katika muziki wa reggae lakini alikuwa anafundisha vijana ili reggae iwe na uendelevu nchini.
Ras Nganyagwa ambaye alitumbuiza kwenye viunga vya Mambo Club iliyopo Ngome Kongwe amesema kwamba amekuja katika tamasha la ZIFF akiwa na mpya nyingi kuonesha wazi kwamba hakuwa mkaa bure.
Akijibu swali kuhusu mahadhi ya muziki wake na imani yake ya kirastafarian amesema kwamba muziki wa rege japo upo ndani ya imani ya kirasta, unasimama wenyewe ndio maana mtu kama yeye hapigi rege ya Jamaica kama ilivyokuwa kwa Jimmy Clief, Burning Spear au Bob Marley.
Amesema muziki wake ni wa kitanzania kwa sababu taifa hili lina vionjo vingi vya kufanya katika kuuza utamaduni wake nje kupitia muziki.
Amesema japo miondoko ya mfumo wa Babylon bado ipo kuna mstari mwembamba sana kati ya dini ya rasta na muziki wa rege na mwitikio wa muziki wa ukombozi.Hata hivyo amesema kwamba sasa hivi anapiga muziki ‘mtamu’ (sweetie reggae) muziki wa mapenzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...