Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na
Teknolojia Profesa Makame Mbarawa 
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imekamilisha rasimu ya miswada mitatu ya sheria za usalama wa mtandao ili kudhibiti uhalifu katika mitandao nchini Tanzania.
Akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo, Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa alitaja miswada hiyo kuwa ni sheria ya usalama wa mtandao, sheria ya kulinda taarifa binafsi, sheria ya miamala ya kielektoniki na shaeia ya kudhibiti uhalifu mtandao na kompyuta.
Alisema rasimu hizo zimewasilishwa kwa mwanasheria mkuu wa serikali ili ziweze kuandaliwa kwa mujibu wa taratibu za uandishi wa sheria.
Pia alisema wizara hiyo imetengeneza kanuni mpya zinazosimamia mawasiliano kupitia mitandao ya simu ambayo ilianza kazi mwezi oktoba mwaka mwaka jana kwa makampuni ya nje kutakiwa kulipa senti 25 za marekani kwa kila dakika moja ya mazungumzo ya simu zinazongia nchini kutoka nje.

Profesa Makame aliongeza kuwa  katika kanuni hiyo mpya imeweka mgawanyo wa mapato hayo ya senti 25 ambapo serikali kupitia hazina inapata senti saba, watoa huduma wanapata senti kumi na tatu na senti tano ni kwa ajili ya uendeshaji wa mitambo ikiwa ni pamoja na kumlipa mwekezaji wa mtambo huo.
Wakati huo huo, mtaalamu wa TEKNOHAMA upande wa usalama wa mtanda Bw. Yusuph Kileo  anabainisha  kwa kuwa sheria mtandao zinatofautiana sana na sheria nyingine,  mapitio yake yanapaswa kufanyika mara kwa mara kutokana na sababu za msingi za makosa mtandao kubadilika badilika kutokana na ukuaji wa haraka wa teknoljia hivi sasa.

 Bw. Kileo anasema uhalifu mtandao umeendelea kukua kwa kasi katika maeneo mbali mbali duniani. Hii imepelekea Microfoft kuanzisha kitengo maalumu kitakacho ongeza uwezo wa kukabiliana na usalama mtandao kama inavyosomeka kwenye taarifa hii “HAPA”.
Wakati huo huo takwimu zilizo tolewa na Idara ya upelelezi kupitia kitengo cha kukabiliana na uhalifu mtandao ya nchini Sirilanka zimeonyesha ukuaji wa makosa hayo katika nchi hiyo yameendelea kukukua kwa kasi. Takwimu hizo zinapatikana katika tovuti yao na kusmeka “HAPA”.
"Pamoja na nguvu kubwa ya mapambano dhidi ya uhalifu mtandao bado changamoto kubwa hasa katika nchi za afrika imekua ni upungufu wa sharia zinazoweza kuwafanya wahalifu kuchukuliwa hatua stahiki pale inapothibitika uhalifu mtandao kufanyika.
"Nchi mbali mbali zimeendelea kuboresha sharia zao na kuzifanya kua kali zaidi ili kuweza kuhimili vishindo vya wahalifu mtandao ambapo wanaonekana kushika kasi ya kipekee. Moja ya nchi hizo ni hapa kwetu TANZANIA", anamalizia Bw. Kileo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...