Assalaamu Alaykum,
Jumuia ya Kiislamu ya An Noor ya Leicester Uingereza inapenda kuwatakia
Waislamu wote mfungo mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Allah akujaalieni nyote afya na nguvu za kutekeleza ibada nyingi zaidi ndani Ya Mwezi huu Adhimu. Pia awape Shufaa ndugu zetu wenye matatizo ya Kiafya na mengineyo. Amin

Jumuia ya An Noor inapenda pia kuwatangazia Waislamu wenzao waishio Leicester Na vitongoji vya karibu kuwa Programu ya Ramadhan InshaaAllah
Itaendelea kama kawaida mwaka huu kwa utaratibu wa Kawaida.
Kila Jumamosi na Jumapili kutakuwa na Darasa za Mwezi wa Ramadhan
Kuanzia Saa Moja na Nusu jioni katika jengo letu 170a Belgrave Gate LE1 3XL Leicester
Baada ya hapo tutakuwa na Futari ya pamoja.
Kama kawaida kila Familia itashiriki katika kuleta futari
Kadhalika kila Familia inakumbushwa kuchangia £5 kila wiki kwa ajili ya Maandalizi.
Programu InshaaAllah itaanza Jumamosi 5/7/2014.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na hawa wafuatao:

Malik 07983614261 au ust Farid 07792174408
au tutumie email: madrasatulnoor.01@gmail.com
Kullu Am Wa Antum Bikhayr


Mohammed Omar, 
Mwenyekiti wa Jumuia 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...