Chama Cha Mapinduzi CCM kimevuna Wanachama wapya Zaidi ya mia moja kutoka chuo Kikuu UDOM.Wanachama hao wapya ambao walipokelewa jana na kupe wakadi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe.Prof.Mark Mwandosya (Prof.Mwandosya ni Mlezi wa Tawi hilo) katika Hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM wamejiunga na tawi la CCM-Elimu (School of Education) UDOM Pichani Mhe.Prof.Mark Mwandosya akizungumza na wanachama wapya wa CCM Tawi la Elimu-UDOM katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM Dodoma.Wengine Pichani ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu(kushoto) na Mwenyekiti wa CCM Tawi la CCM-Elimu-UDOM Bw.James Martin aliyekaa katikati.
Wanachuo wakimsikilizaMhe.Prof.Mark Mwandosya
Mhe.Prof.Marck Mwandosya akiwa makao makuu ya CCM akisindikizwa na wanachama wa CCM Tawi la Elimu-UDOM mara baada ya kupokea wanachama wapya zaidi ya miamoja.
Wanachama wapya wa CCM ambao walipokelewa jana na kupewa kadi na Mhe.Prof.Mark Mwandosya katika Hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa NEC Makao Makuu ya CCM wamejiunga na tawi la CCM-Elimu (School of Education) UDOM wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri.
Na Deusdedit Moshi Mtendaji Mkuu wa Photo Solutions wawakilishi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati. Picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...