Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)  leo limesaini mkataba na Halmashauri ya Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya ya Ujenzi wa Nyumba 5,000 za gharama nafuu.
Utiaji saini makubaliano hayo umefanyika leo mchana katika Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Wabunge wanaotoka Mkoa wa Mbeya wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum)  Mhe.Prof Mark Mwandosya, ambaye Wilaya hiyo Mpya iko katika Jimbo lake la Rungwe Mashariki,  na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Mhe.Aggrey Mwanri.
 Pichani wanaosaini kuanzia kulia ni kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC,Bwa.Felix Maagi,Bw.Meckson Mwakipunga (M/Kiti wa Halmashauri  ya Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya na Bw. Said Mderu.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC,Bwa.Felix Maagi akibadilishana Mkataba  na M/Kiti wa Halmashauri  ya Wilaya Mpya ya Busokela Bw.Meckson Mwakipunga  baada ya kutiliana  saini Ujenzi wa nyumba 5,000 katika Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya .
 Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya Mpya ya Busokela Bw.Meckson Mwakipunga akielezea kuhusu Mradi mzima,  baada ya kutiliana  saini Ujenzi wa nyumba 5,000 katika Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya .
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Mhe.Prof Mark Mwandosya. Waziri ambaye Wilaya hiyo Mpya iko katika Jimbo lake la Rungwe Mashariki akitoa shukurani baada ya mkataba  wa Ujenzi wa Nyumba 5,000 za gharama nafuu kusainiwa.
Baadhi ya Wabunge wanaotoka Mkoa wa Mbeya wakifuatilia  utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa nyumba 5,000 za gharama nafuu katika Halmashauri ya Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya .Na Deusdedit Moshi Mtendaji Mkuu wa Photo Solutions wawakilishi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2014

    Gharama nafuu ni kiasi gani na nymba ya ukubwa gani??!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...