Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania –TRL unasikitika  kuwataarifu wananchi na wateja wake  wa  huduma ya treni ya Jiji kuwa hiyo  imesitishwa kwa muda wa siku 3 kuanzia kesho Juni 19, 2014 hadi  Jumammosi Juni 21, 2014. Aidha huduma hiyo itaanza tena hapo Jumatatu Juni 23, 2014 kwa kufuata ratiba yake ya kawaida.
Uamuzi huo unatokana na sababu za kiufundi ikiwemo kufanyiwa matengenezo vichwa vyote vya  viwili ambavyo vimekuwa vikihudumia treni hiyo ya Jiji. Vichwa hivyo vinapaswa kufanyiwa ukarabati katika Karakana Kuu ya TRL Morogoro na kwamba vitarejeshwa Jijini Jumapili Juni 22, 2014.
Uongozi wa TRL inawaomba radhi wananchi na wateja wake wote jijini kwa usumbufu utakaojitokeza.
-Tamati-
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ,
Mhandisi  Elias Mshana
Dar es Salaam,
Juni 18, 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...