100.5 Times Fm Radio imetoa kiasi cha shilingi milioni tatu kwa albino wa wilaya ya Temeke, Dar es Salaam kama sehemu ya mchango wao kwa jamii hiyo yenye ulemavu wa ngozi inayokumbwa na changamoto nyingi.

Katibu wa Kampuni ya Times Fm Radio, Amani Joachim ameukabidhi uongozi wa chama hicho hundi halisi akiwa ameambatana na Aluta Warioba (Meneja Vipindi Msaidizi) na Mzee Chapuo kutoka katika idara ya ubunifu.

Amani Joachim aliwaomba wapokee kiasi hicho kwa kuwa bado Times Fm itaendelea kushirikiana nao katika kupambana na changamoto zinazowakabili na kuhamasisha jamii kuendelea kuonesha upendo kwa walemavu.

Baada ya kupokea hundi halisi ya kiasi hicho cha fedha, mwenyekiti wa chama cha Albino Temeke, Khasim Kibwe alitoa shukurani zake kwa chombo hicho cha radio na kueleza kuwa fedha hizo zitasaidia sana katika kununua mafuta maalum ya ngozi kwa wanachama wake.

“Kwanza nafurahi sana kwa kutujali sisi Albino. Lakini vilevile wito kwa jamii nao waige mfano huu wa 100.5 Times Fm nao waweze kuwachangia watu wenye albinism. Baada ya kuwa kiongozi, nakumbuka hata mlipotushirikisha katika mpira mwaka 2008 tuliona urafiki wenu wa karibu, vilevile sasa tunauona urafiki wenu umekamilika zaidi. Ni watu ambao mnajali watu wenye mahitaji maalum.

“Jamii iendelee kusikiliza Times Fm na wale wenye mahitaji wengine basi waipende Times kwa kuwa inapenda watu wa aina zote.” Amesema bwana Kibwe. Viongozi wengine wa chama hicho waliokuwepo ni pamoja na muweka hazina, Said Ndonge na katibu wa chama, Gaston Mcheka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...