Kwa wasanii wao kila usemi ni sehemu ya maisha yao! Juzi baadhi ya wasanii huko Ughaibuni
wameibuka kwa kuyabandika majina mazoezi ya kukata uzito au unene wa mwili " Zoezi
hili sasa lipewa jina la "UZEE MWISHO CHALINZE" usemi ambao umebuniwa na msanii Joti wa Ze Komedi. Zoezi hilo maalumu la kupiga vita unene au minyama ya uzembe
limeshaanza kufanyiwa kazi kisawa sawa na wasanii,mmojawapo ni mwanamuziki
Jhikoman ambae kwa sasa ana ziara ndefu huko Ulaya
Mwanamuziki Jhikoman akijifua kupiga vita unene huko ughaibuni
Hii ndio maana mwanamuziki Jhikoman huwa hachoki awapo jukwaani
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...