Wafanyakazi wa Citi Bank tawi la Tanzania wameweza kujichangisha wenyewe kwa wenyewe na kupata fedha zilizofanikisha ukarabati wa jengo litakalotumika kama jiko la kupitia na ukumbi wa kulia chakula kwenye Kitengo cha Watoto wenye Ulemavu wa akili cha Shule ya Msingi Tandika,Wilayani Temeke jijini Dar es Salaam,Wafanyakazi hao wameamua kufanya hivyo leo ikiwa ni muendelezo wa mpango wao wa kusadia watu wenye Mahitaji,wanaofaunya mara moja kwa mwaka Duniani kote,mbali na ukarabati huo waliweza pia kujitolea kufanya usafi wa Mazingira ya eneo la Shule hiyo.
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Citi Bank tawi la Tanzania wakiwa wamejumuika pamoja na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tandika ambao wanaulemavu wa Akili.
Wanafunzi hao wakifurahia ugeni huo uliowatembelea leo.
Meneja Mkuu wa Citi Bank tawi la Tanzania,Noel Sangiwa (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Watoto wenye Ulemavu wa Akili Tandika,Mary Batamula (katikati) wakishirikiana kukata Utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa jengo litakalotumika kama jiko la kupitia na ukumbi wa kulia chakula kwenye Kitengo cha Watoto wenye Ulemavu wa akili cha Shule ya Msingi Tandika,Wilayani Temeke jijini Dar es Salaam leo.
Sehemu ya Wafanyakazi wa Citi Bank tawi la Tanzania wakifanya usafi wa Mazingira katika eneo la Shule ya Msingi Tandika ambako kuna Kitengo cha Watoto wenye Ulemavu wa Akili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...