Washiriki wakifuatilia Majadiliamo katika Kongamano la  Kukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani la Mwaka 2014 ambapo "Vijana Wetu, Hazina Yetu" ndio  Kauli Mbiu ya Mwaka huu.
 Dr. Salha Mohamed akichangia mada kuhusu hali za Vijana Mayatima na Jinsi Jamii ya Kitanzania inavyoshindwa kuwaangalia na kuwaokoa na Changamoto za Dunia ya Leo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Prof Mohamed Badamana akifafanua jinsi gani Malezi na Maadili Bora ya Vijana yanaweza kuwa Chachu ya Nchi zetu za Kiafrika kupiga hatua za Maendeleo ya haraka.
 Bro Ali Masoud AKA Masoud Kipanya Akitoa mada ya Umuhimu wa kufahamu Kuwasaidia vijana kuwa na Fikra Kubwa kuwawezesha Kumfahamu Mungu na Mazingira Yao Kuleta Maendeleo ya Jamii na Nchi.
 Washiriki wa Kongamano la Kukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Wakimsikiliza kwa Makini Sheikh Mussa Kundecha alipokuwa akielezea Usomaji Qur'an, Ushiriki wa Katiba ya Nchi na Hatima ya Vijana.
 Wanataaluma wa Kiislam wakifuatilia kwa makini Mjadala wa Nafasi ya Vijana na Maendeleo ya Jamii ya Kitanzania Miaka Ijayo Katika Ukumbi wa JNICC - Dar es Salaam.
 Prof Mohamed Badamana wa Chuo Kikuu Cha Nairobi, Dr. Mohamed Mohamed Said, Mwanahistoria wa Tanzania na Sheikh Khaled Mtwangi wakibadilishana Mawazo wakati wa Kongamano la Kuukaribisha Mwezi Mtukufu.
 Washiriki wakiwa na Furaha Kwa Kujaaliwa Kushiriki Kongamano la Ramadhani Ambalo zaidi ya Wanataaluma  na Wanazuoni 700 walikutana na Kujadili nafasi ya Vijana na Mustakabali wa Nchi.
Baadhi ya Wanataaluma Washiriki wa Kongamano la Kukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wakati wa Mapumziko na Kubadilishana Mawazo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 23, 2014

    alhamdulillah

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 23, 2014

    Ni kwa madhumuni gani waislam wakuatane na kujadili mambo ya taifa ikiwa serikali ipo ? Au wanamipango ya kuigeuza Tanzania kua nchi ya Kiislam ?

    Mpenda Nchi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...