Washindi wa bahatinasibu ya Shinda Ki-Brazili na Mwanaspoti,Issa Rashid (wapili kushoto) na Michael Msumba (wapili kulia) wakipokea zawazi zao kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Mult Choice ( Dstv ) Barbara Kambogi (kulia) na Afisa Masoko wa Kampuni ya Mwananchi,Edward Uisso.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Mwananchi,Edward Uisso (wapili kushoto) akiongea na Mshindi wa promosheni ya Shinda Ki-Brazili na Mwanaspoti,wakati wa kuchezesha droo ya wiki ya pili, kulia ni Afisa Uhusiano wa Mult Choice (Dstv ) Barbara Kambogi.

Kampuni ya Mwananchi Communications Limited kupitia gazetilake la michezo la Mwanaspoti kwa kushirikiana na DSTV wamekabidhi zawadi za washindi wa kwanza wa ptomosheni ya Shinda Ki-Brazil iliyozinduliwa wiki iliyopita.

Washindi walizawadiwa ni Michael Namenga, Issa Ndingo na Christopher Chengulla ambao walizawadiwa ving'amuzi na vifurushi vyake huku Jackson Fredrick wa Mwanza akikabidhiwa jozi ya jezi yenye jezi 16.

Mbali ya kukabidhi zawadi hizo, promisheni hiyo pia iliendesha droo na kupata washindi wapya. Washindi wa vingamuzi vya DSTV pamoja na kifurushi kizima cha malipo kwa mwezi mmoja (Compact Plus) waliopatikana ni Sharifu Migui (34) ambaye ni Fundi Magari, John Kilalago (39) ambaye ni Mlinzi, Mahmud Salum (54) ambaye ni Mtaalamu wa Takwimu wakati mshindi wa jozi moja ya jezi(ina jezi 16) ni Bariki Massawe(38) ambaye kazi yake ni mfanyabiashara.

Migui ambaye ni mkazi wa Mikumi Morogoro alisema, " Ninafuraha kushinda kwenye shindano hilo. Ni kitu rahisi kupata kama mtu unashiriki kwani unakuwa umejijengea nafasi ya kutosha endapo ninashiriki na mimi nimeshiriki mara nyingi ."

Massawe ambaye ni mkazi wa Tabata Kinyerezi alisema," Nimefurahi kushinda jezi baada ya kushiriki kwenye promosheni bomba ya Mwanaspoti. Jezi hizo nitatoa zawadi kwa timu yangu ya maveterani inayoitwa Kinyerezi Veteran FC."

Afisa Masoko wa Kampuni ya MCL, Edward Uisso, amesema kuwa bado kuna zawadi nyingi zimebaki kwa wasomaji ambazo ni runinga tatu zenye ukubwa wa inchi 32, dekoda 24 za DSTV zilizounganishwa na kifurushi cha Compact Plus kwa muda wa mwezi mmoja, seti nne za jezi pamoja na fedha taslimu zinazotolewa kila siku mpaka shindano litakapomalizika.

Promosheni hiyo ambayo ilifunguliwa Juni 2 itafungwa Julai 13 siku ya mwisho ya fainali hizo.Ili kuendelea kushiriki, wasomaji wa Mwanaspoti watatakiwa kutuma namba zitakazopatikana kwenye ukurasa huu wa tatu wa gazeti la Mwanaspoti kwenda namba 15551.

Kwa mujibu wa vigezo na masharti ya promosheni hiyo, kila nakala ya gazeti la Mwanaspoti itakuwa na namba mbili za ushiriki zenye tarakimu nane kila moja.

Mshiriki ana hiari ya kutuma namba yoyote kati ya hizo kushinda aina moja ya zawadi, au akipenda anaweza kutuma namba zote mbili ili kujishindia aina zote mbili za zawadi.

Namba moja imetambulishwa kwa herufi B na itamwezesha mshiriki kuingia kwenye droo ya zawadi za binafsi. Namba ya pili imetambulishwa kwa herufi T na itamwezesha mshiriki kuingia kwenye droo ya zawadi za timu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...