Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kushoto), Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu (kushoto), Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile (wanne kushoto) wakipokea taarifa kuhusu Mfumo wa Ufuatiliaji wa Mienendo ya Watu (Public Surveilance Sytem (Global eye)  kutoka kwa Mtaalam wa Kampuni ya Telecom ya nchini China. Waziri Chikawe na ujumbe wake wapo jijini Beijing, China kwa ziara ya kikazi. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Kampuni ya Kutoa Huduma ya Mawasiliano nchini China, Li Ping alipokuwa akimfafanulia masuala mbalimbali ya mawasiliano yanayofanywa na Kampuni yake. Waziri Chikawe yupo jijini Beijing nchini humo na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu, Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile kwa ajili ya ziara ya kikazi. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kushoto), Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu, Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya Kutoa Huduma ya Mawasiliano nchini China, Li Ping. Waziri Chikawe na ujumbe wake wapo jijini Beijing, China kwa ziara ya kikazi. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...