"Ohoooooo.... Gari langu maskini...." Dereva wa teksi anatoka nje kuangalia jinsi gari lake lilivyoingia kwenye chemba ya maji machafu ambayo mfuniko wame umeeshaenda kusikojulikana na kuacha shimo kubwa katikati ya barabara ya Mtaa wa Zanaki jijini Dar es salaam leo
 Wasamaria wema wanasogea kuja kumuokoa
 "Hayaaaa....twendeeeeee" Gari linatoka
 Anapiga rivasi taratibu huku mshimo ukiwa umeachama  
Anaondoka taratibu huku akisikitika na kujiuliza nini kifanyike kuondoa adha hii jijini....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 22, 2014

    Yaani huyu dereva hakuliona hilo shimo??

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 22, 2014

    Wahusika watafute mifuniko mbadala kama ya zege badala ya chuma kuondokana na hii kero

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 22, 2014

    Ama kweli hii dunia ina tofauti kubwa kati ya nchi na nchi. Shimo kama hili lingeoneka huku nchi za wenzetu basi angeshitakiwa mkuu wa jiji lakini huko kwetu linaonekana kama ni jambo la kawaida sana na dereva anaondoka kama hakuna kitu kilichotokea.Any way kidogokidogo nasi tutafika tu oneday

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 22, 2014

    Huyo mdao hapo juu anikumbusha mbali sana. maana miaka hiyo niliwahi kutumbukia kwenye shimo kama hilo, na gari langu likapata uharibifu kweli. Kisha nikazungukwa na wajanja, mmoja wao takribani miaka mitano ama sita hivi, kisha kajaa mafua, akaniambia, hukuliona hilo shimo, wewe kipofu nini.He just made my day.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...