Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe akizungumza na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Kata ya
Namikango, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi leo.
Waziri Chikawe aliwataka
viongozi hao kuwa na umoja ili kukipa nguvu chama chao hasa katika kipindi hiki
wanapoelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo kila mwanachama wa
chama hicho alisisitizwa kuchukua fomu wakati muda utakapofika wa kuchukua fomu
hizo.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka
huu ambapo wananchi watachagua Viongozi wa Mamlaka za Wilaya, Mamlaka za Miji
midogo, Mamlaka za Miji na Halmashauri za Vijiji na Vitongoji. Kulia ni
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nachingwea, Albert Mnali. Picha na Felix Mwagara wa WMNN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...