IMG-20140704-WA0013Waziri wa Maliasili na utalii Mh. Lazaro Nyarandu akifungua rasmi mkutano wa 30 wa asasi ya wamiliki wa makampuni ya kusafirisha watalii TATO jijini Arusha hivi karibuni. 
IMG-20140704-WA0009Wadau mbalimbali wa utalii wakisikiliza mada kwa umakini
IMG-20140704-WA0004
MAKAMPUNI ya kitalii hapa nchii yametakiwa kuutangaza kwa kiasi kikubwa utalii wa vivutio vyetu hapa nchini  ndani ya nchi pamoja na nje ya nchi ili kuwapa wanachi moyo wa kizalendo katika kujali vivutio walivyo navyo.
 
Hayo yalisemwa juzi jijini Arusha na waziri wa Maliasili na utalii Mh. Lazaro Nyarandu wakati akifungua mkutano wa 30 wa asasi ya wamiliki wa makampuni ya kusafirisha watalii TATO ambapo  alisema kuwa hii ndio nafasi kubwa waliyokuwa nayo makampuni hayo makubwa ya uendeshaji shughuli za kitalii.
 
Pamoja na hayo pia ameyataka makampuni hayo ya kitalii kuhakikisha yanaongeza kiasi kikubwa cha watalii wanaoingia hapa nchini ili kuingizia serekali fedha nyingi za kigeni na kuachana na kasumba iliyozoeleka ya kupandisha ada ya kiiingilio cha katika hifadhi zetu pamoj a na vivutio.
 
Aidha kwa upande wa kutunza utalii wa Utamaduni Waziri wa maliasili mh. lazaro Nyarandu amezitaka kampuni hizo zinazohusika na kuwa shafirisha watalii katika mbuga kuhakisha wanawapitisha watalii katika sehemu za kiutamaduni kwa maana kama wanyama watalii wameshawaona na upande wa utamaduni nako kuna ulazima mkubwa sana.
 
Pia Waziri wa maliasi na utalii alisema kuwa kwa sasa wizara yake imejipanga katika kutangaza utalii hapa nchini na sasa hivi wanaanza kutangaza katika shirika katika mashirika makubwa ya habari kiwemo Shirika la hababri la BBc pamoja na CCN.
 
Naye Mwenyekiti wa TATO Bw. Willey Chambulo ametoa malalamiko yake kwa serekali na kuwakilisha kwa waziri wa Maliasili Mh. Lazaro Nyarandu kuhusiana na tatizo la hivi karibuni la kuwepo kwa mageti yasiyo rasmi katika baadhi ya hifadhi hapa nchini.
 
Alisema kuwa, hii imetoke hivi karibuni katika mbuga ianayomilikiwa na TANAPA mnamo tarehe 01 mwezi huu na kudaiwa ongozeko la kodi amabalo wao hawakuwa  taarifa na hivyo kuwapa usumbufu kupelekewa kukamatwa kwa watalii waliokuwepo kuzuiliwa na kuwekwa chini ya Ulinzi hivyo kupelekea kurudisha nyuma hali ya utalii hapa nchini.
 
Hata hivyo Waziri wa Maliasili Mh. lazaro Nyalandu  alijibu malalamiko hayo kwa kusema kuwa akiwa kama waziri mwenye dhamana ameshatoa maagizo kwa mamlaka zote za uhifadhi pamoja na mbuga kusitisha mara moja kusumbua watalii na kuwataka kutumia lugha nzuri katika kudai mapato.
 

Mkutano huu wa TATO wa 30 unatarajiwa kupitia Mahesabu yaliyopita pamoja na kufanya uchaguzi wa kuchagua viongozi wapya wa Asasi hiyo.(Pamela Mollel wa jamiiblog).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ankal, katika kublogu kwa miaka kadhaa, nimethibitisha kuwa blogu ina nafasi katika kutangaza utalii. Makala mbili tatu nilizoandika katika blogu yangu ya ki-Ingereza, kuhusu Mbambabay, Lushoto, na hasa moja iitwayo ""Tourism in Longido," zinatembelewa sana na wadau kutoka sehemu mbali mbali duniani.

    Mfano hai: Wajerumani fulani waliniandikia, kutokana na waliyosoma kwenye blogu yangu kuhusu Mbambabay, nikawa mshauri wao katika kupanga safari ya Mbambabay. Walisafiri.

    Kwa hivi, pamoja na kutambua na kupongeza mchango wa makampuni ya utalii katika kutangaza vivutio, hata blogu inaweza kutoa mchango fulani, katika huu utandawazi na teknohama.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...