Naibu Waziri wa Maji,Mh. Amos Makalla (kulia), akipata maelezo kutoka kwa kiongozi wa Mafundi wa Kampuni ya CDM Smith, John Donoherth, kuhusu ujenzi wa kisima kilichopo Mkwalia Mkuranga ambacho ni moja kati ya visima 8 vinavyofanyiwa utafiti maji wilayani humo. Makalla alifanya ziara ya kukagua miradi ya maji wilayani Mkuranga mkoani Pwani leo. Pia alikagua mradi wa kisima cha maji cha Nyamato chenye uwezo wa kutoa maji lita 26,000 kwa saa kitakachohudumia wakazi wa vijiji vya Mvuleni, Nyamato na Kilimahewa.
Naibu Waziri wa Maji, Mh. Amos Makalla akiangalia mradi wa kisima cha Mkwalia ambacho kinafanyiwa utafiti
Maji yakitiririka kwenye kisima hicho
Naibu Waziri wa Maji, Mh. Amos Makalla akijadiliana jambo na Mkandarasi wa kisima hicho,John Donoherth
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...