Waimbaji nyota wa muzki wa Injili,Anastazia Mukabwa akiwa amepozi na Rose Muhando.

MWIMBAJI nguli wa muziki wa Injili nchini Kenya, Anastazia Mukabwa, ni miongoni mwa wakali ambao mwimbaji Rose Muhando anatamani wawepo kwenye uzinduzi wa albamu yake ya Kamata Pindo la Yesu.
 
Rose Muhando amepanga kuzindua albamu yake ya Kamata Pindo la Yesu Agosti 3, mwaka huu ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam.
 
Akizungumza na gazeti hili, Muhando alisema Mukabwa aliyemshirikisha katika wimbo wa Vua Kiatu ni aina ya wasanii wenye uwezo mkubwa wa kuimba na kwamba tayari ameiomba Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi wake iwasiliane na msanii huyo kuhakikisha anapatikana siku hiyo.
 
“Wapo waimbaji wengi wa Injili natamani wawepo siku hiyo, lakini ningefurahi kama ningempata Anastazia Mukabwa wa Kenya, hivyo tayari nimeiomba Kamati ya Maandalizi ifanye kila iwezalo aje.
 
“Ni aina ya uzinduzi wa pekee ambao nataka ufanyike siku hiyo, ni imani yangu tutampata Mukabwa na wakali wengine,” alisema na kuongeza kuwa ujio wa Mukabwa utakuwa mzuri ili mashabiki 'wavue viatu' siku hiyo.

Nyimbo zilizopo katika albamu ya Kamata Pindo la Yesu ni Bwana Niongoze, Wewe Waweza, Usiniache, Nibariki, Muongo, Kwema, Kamata Pindo la Yesu na Facebook.


Hivi sasa Rose anatamba na albamu yake ya Utamu wa Yesu yenye nyimbo saba, ambapo albamu zake nyingine ni Uwe Macho, Nyota ya Ajabu (Zawadi ya Krismasi), Jipange Sawasawa, Kitimutimu, Mungu Anacheka na Wololo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...