Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) umetangaza kukipeleka kwenye matengenezo makubwa kivuko cha Mv Kigamboni, kinachotoa huduma ya kuvusha watu na magari kwenda na kurudi Kigamboni jijini Dar es salaam.
Aidha huduma za uvushaji watu pamoja na magari zitaendelea kutolewa na vivuko vya Mv Magogoni pamoja na Mv Lami katika kipindi chote cha matengenezo husika. 
Ofisa Habari wa Temesa, Theresia Mwami alimwambia mwandishi jana kuwa wakala huo unaomba radhi kwa usumbufu ambao wananchi wanaotumia vivuko watakaoupata wakati kivuko hicho kitakapokuwa kwenye matengenezo. 
Mwami alisema vivuko hivyo havijafanyiwa matengenezo makubwa kwa muda mrefu hivyo kitafanyiwa matengenezo kivuko cha Mv Kigamboni kwanza na baadae Mv Magogoni. 
Alisema kivuko cha Mv Lami kina uwezo wa kuchukua abiria 100 na magari madogo 16 wakati kivuko cha Mv Kigamboni kinachukua magari 23 na abiria 800.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...