Kutoka Arusha taarifa zinasema msako mkali unaendelea kufuatia shambulio la bomu la mkono alilotupiwa  Sheikh wa msikiti wa Qiblatan Sood Ally Sood (37) uliopo eneo la Kilombero jijini Arusha  wakati akila daku.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo imedaiwa kuwa Sheikh huyo amejeruhiwa sehemu mbalimbali ikiwemo miguu yake yote miwili sehemu za mapajani pamoja na Kifuani na kupoteza baadhi ya vidole vya miguu yote miwili.
Mbali na Sheikh huyo pia kuna mtu mwingine aliyekuwa nyumbani kwake hapo aliyetajwa kwa jina la Muhaji Kifea (38) ambaye ni mkazi wa Dar es salaam naye amejeruhiwa na wote wamelazwa katika hospital ya mkoa Mount Meru kwa ajili ya matibabu.

Akizungumza hospitalini hapo sheikh Sood amesema tukio hilo lilitokea nyumbani kwake eneo la majengo ya chini ,usiku wa kuamkia leo majira ya saa 5 wakati yeye pamoja na mgeni wake walikuwa wakila chakula sebuleni Amesema alishangaa kusikia mlio mkubwa ulioambatana na vyuma mbalimbali vilivyokuwa vikiruka hewani ,ambapo bomu hilo linaelezwa kuwa ni guruneti lililorushwa kupitia dirishani baada ya watu wasiofahamika kufanikiwa kuvunja kioo cha dirisha la chumbani katika nyumba hiyo. 

Ameongeza kuwa wahusika wanafahamika maana walishawahi kumtishia kupitia waraka wa maandishi pamoja na kumfyatulia risasi.
 Amesema kuwa siku tatu kabla ta tukio hilo alikoswakoswa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika wakati akitoka msikitini na kutoa taarifa katika kituo kikuu cha polisi jijiji hapa juu ya tukio hilo. 

Sheikh Sood, ambaye ni kiongozi Alswasun kanda ya kaskazini, inasemekana amekuwa akitofautiana na waamini wenzake kutokana na msimamo wake mkali wa kutokukubaliana na makundi ya kigaidi yanayojiita jihadi yanayotokana na vijana wenye msimamo mkali.

 Inahofiwa waliofanya udhalimu wanahusika na vikundi vya ugaidi na kwamba  wanasakwa hivi sasa na vyombo vya ulinzi na usalama. Tutaendelea kuwapasha taarifa zaidi kwa kadri zitavyopatikana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...