AZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema rasimu ya Sera ya Diaspora iko kwenye hatua za mwisho za maandalizi na muda si mrefu itaingizwa kwenye utaratibu wa Kiserikali ili hatimaye iweze kuwasilishwa kwenye Baraza la Mawaziri.

Akizungumza na Watanzania wanaoishi Uingereza kwenye mkutano uliofanyika ubalozi wa Tanzania jijini London mwishoni mwa wiki, Waziri Mkuu alisema mchakato wa kuandaa rasimu hiyo ulihusisha wadau wengi kwa kadri ilivyowezekana ili kupata wigo mpana wa suala zima la diaspora.

“Katika hatua za awali, mbali ya ofisi yangu na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, tuliwashirikisha kwa karibu Umoja wa Wanadiaspora waliorudi Tanzania (Tanzania Diaspora Initiative) na wanadiaspora kutoka Uingereza, Marekani, China, Oman, India na Afrika Kusini ili kupata uzoefu wao kutokea huko waliko,” alisema na kuongeza:

“Baadaye tukawapelekea wataalamu ambao ni Profesa Samuel Wangwe wa REPOA, Profesa Joseph Semboja wa Uongozi Institute na Profesa Faustine Kamuzora wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kila mmoja kwa wakati wake na kuwaambia waichanechane kadri wawezavyo na kisha watupe mrejesho wao.”

Aliwataja wadau wenginu muhimu waliohusishwa kwenye kuichambua rasimu hiyo kuwa ni Shirika la Kimataifa linaloshughulika na Wahamiaji (International Organisation for Migration –IOM) ambao wamebobea katika masuala ya wahamiaji katika nchi mbalimbali duniani. 

“Kwa mtazamo wangu hii rasimu imekaa vizuri kwa sababu tumejitahidi kugusa kila eneo ambalo kwenu lilikuwa na umuhimu wa kipekee. Sasa hivi imeshawekwa vizuri kimfumo na inasubiri iingie katika utaratibu wa kiserikali,” alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...