Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma akimvisha kofia ya ukamanda Profesa Peter Msolla baada ya kuteuliwa kuwa Kamanda wa UVCCM wilaya ya Kilolo sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Kidabaga. 
 Mbunge wa jimbo la Kilolo,Profesa Peter Msola akila kiapo cha kuwa kamanda wa UVccm mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma.
 Mbunge wa jimbo la Kilolo,Prof Peter Msola akiwaapisha makamanda wa vijana ccm katika wilaya ya Kilolo sherehezz ilizofanyika katika uwanja wa Kidabaga.

Na Denis Mlowe,Kilolo

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana  Chama  cha Mapinduzi (CCM)  Taifa, Sadifa Juma Hamis ametoa rai kwa   vijana kuepuka kutumika katika kuvuruga amani na utulivu uliopo nchini Tanzania kwa kutumika na baadhi ya vyama vya siasa na kuhatarisha amani  ya Taifa.
 
Sadifa alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki katika  viwanja  vya Kidabaga wakati akiwahutubia wananchi  wa Kidabaga kata ya Bomalang’ombe wilayani Kilolo wakati wa kusimikwa kwa mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msola kuwa kamanda wa umoja wa vijana CCM wa wilaya ya hiyo.
Alisema kuwa amani  ambayo tunajivunia  ipo  siku  itatoweka  na iwapo  vyama  vya siasa  vitaacha kufanya kazi yake ya  kisiasa kwa kunadi  sera  za vyama  vyao na kueneza  chuki  dhidi ya  serikali kama ilivyo  hivi  sasa kwa baadhi ya  vyama kuendesha siasa  za  chuki na  kuwatumia vijana kuvuruga amani yetu.
 
" Nawaombeni  sana vijana  wa   kuendelea   kuonyesha mfano  kwa  vijana  bora katika kudumisha amani iliyopo na kamwe msije iga siasa vya vyama  vya upinzani siasa ya  kufanya  vurugu ..... hiyo ni siasa mbaya  sana na itakuja  kuliweka Taifa katika umwagaji damu ambao hakika itakuwa ngumu sana kuweza kuishi tena kama mwanzo” alisemaSadifa
 
Alitoa mfano kuwa kuna ushahidi kwa nchi jirani unaonesha madhara ya kuichezea amani na kuongeza kuwa ni rahisi sana kupoteza amani na umoja lakini ni vigumu sana kuirejesha na kuwataka vijana kuacha kuandamana kwa kuiga tu kwa kuwa umeambiwa fanya jambo hilo
 
Mbali ya kuwataka  vijana kuacha kutumiwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa Sadifa aliwataka viongozi  wa vyama  vya siasa kutowatumia vijana hao  katika kuvuruga amani pia aliwataka vijana kutokubali siasa  chafu zenye chembe ya vurugu kwa watanzania na kuongeza kuwa sehemu yoyote yenye amani na utulivu, yapo maendeleo kwa sababu wananchi wanafanya shughuli za maendeleo kwa uhuru
 
 Kwa upande wake Kamanda mpya wa umoja wa vijana Ccm wilaya ya Kilolo, Prof Peter Msola aliwataka vijana kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuondokana na umaskini katika wilaya hiyo na kuwataka kushirikiana katika kudumisha amani iliyopo nchini Tanzania.
 
Alisema moja changamoto kubwa inayowakabili vijana na ambayo kwa kushirikiana nao atahakikisha inafanyiwa kazi kwa kutumia fursa mbalimbali zinazowazunguka ni ajira kwa kuwa fursa hizo zinaweza kuwa  katika sekta ya biashara, kilimo na ushauri kwa kupitia vikundi vya maendeleo.
 
Alisema ardhi na hali ya hewa nzuri ya wilaya ya Kilolo inaweza kuwaongezea fursa ya ajira vijana wa wilaya hiyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...