Mkuu wa Morogoro Joel Bendera akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.
  

 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akikagua timu wakati wa uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.


Bendera atilia mkazo soka la vijana.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera, atilia mkazo soka la vijana na kuwataka viongozi wa mpira wa miguu mkoa wa Morogoro na chama cha mpira wa miguu Tanzania kutilia mkazo program za vijana.

Kocha wa zamani wa timu ya Taifa – Taifa Stars atoa changamoto wakati akifungua mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Morogoro siku ya jumanne. Alisema kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya mpira wa miguu zaidi ya kuwekeza katika shule za soka na programu za vijana kama Airtel Rising Stars. Awapongeza  Airtel kwa mchango wao.

Zaidi ya majuma mawili kumekua na maoni ya kutoka kwa wakuu wa mikoa na wadau wengine wakisisitiza viongozi wa mpira wa miguu nchini kutilia mkazo programu za vijana kuiwezesha Tanzania kufanya vizuri.

Wakifungua mashindano ya Airtel Rising Stars katika mikoa yao hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Said Meck Sadiki na Mkuu wa mkoa Mbeya Abbas Kandoro nao walitilia mkazo kuwekeza katika mpira wa vijana. Wengine waliotoa maoni hayo ni meya wa Mwanza Stanslaus Mabula na Mbunge wa Ukonga Eugen Mwaiposa.

Mashindano ya Airtel Rising Stars yanaitimishwa leo (August 7) na timu zinatarajiwa kuwasili jijini Dar-es-Salaam siku ya jumamosi August 9 katika fainali za taifa ambazo zinaanza kutimua vumbi jumapili katika kiwanja cha kumbukumbu ya Karume. Fainali za Taifa zitamalizika tarehe 17 August na wachezaji wakiume na wa kike watakao chaguliwa wataweka kambi jijini Dar-es-Salaam wakijiandaa na mashindano ya kimataifa Airtel Rising Stars yatakayofanyika nchini Gabon.

Mwaka jana mashindano hayo yalifanyika nchini Nigeria na timu ya wasichana ya Tanzania walinyakua ubingwa na kuzawadiwa dollar za marekani 10,000.   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hahahaha isipokuwa Kiongozi Mkuu wa Mkoa Joel Bendera mmemvalisha ngozi ya chui kwa Fulana ya Airtel (Nyekundu) Msimbazi wakati yeye ni Yanga!

    ReplyDelete
  2. Huyu alipelekwa kusomea kandanda ujerumani ya Magharibi ili aje kunyanyua soka la bongo. Alikochi timu ya taifa kidogo alivyorudi ila naona hela ipo kwenye siasa. Kila mtu mwanasiasa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...