Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe
(kulia) akimuapisha Afisa Utumishi wa wizara hiyo, Anna Yusufu Mariam kuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Jeshi
la Polisi na Magereza inayoshughulikia masuala ya Utumishi na Utendaji wa
askari wa majeshi hayo, katika Ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia
ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima, na kushoto ni
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akimpa
hati ya kiapo Afisa wa Jeshi la Polisi, Jonas Mugendi baada ya kumuapisha kuwa Mjumbe
wa Sekretarieti ya Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza jijini Dar es Salaam
leo. Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima, na
katikati ni Katibu Mkuu, Mbarak Abdulwakil. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe
(kushoto-meza kuu) akiongoza kikao cha Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza
inayoshughulikia masuala ya kiutumishi na kiutendaji wa askari katika Majeshi
hayo, katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo
ya Nda ni ya Nchi, jijini Dar es Salaam leo. Kulia Meza Kuu ni Naibu Waziri wa
Wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Picha zote
na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
PICHA ZOTE NA KITENGO CHA
MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA
NCHI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...