Takaful ni bima inayofuata maadili ya ki- Islam ambayo inatofautiana na bima isiyofuata maadili hayo ktk baadhi ya sifa zake. Fikra ya takaful inatokana na ukweli kwamba swala linalomsumbua mtu mmoja mmoja ktk maisha, linaweza kuwasumbua watu wengi, kama watu wale wataamua kushirikiana ktk kutatua tatizo lao kwa pamoja, basi wote wanaweza kufaidika.

Kuna tofauti za msingi kati ya bima inayofuata maadili ya ki -Islam na ile isiyofuata maadili ya ki-Islam. Ktk kulifafanua hilo wataalam wa takaful wanaeleza kwamba takaful sio mkataba wa biashara ambapo mmoja anauza na mwengine ananunua, ispokua ni utaratibu unaopangwa na kikundi cha watu wenye malengo yanayofanana na wakaahidi kuwa  watashirikiana endapo mmoja wao atapatwa na tatizo. Watu hao wanachanga pesa zao (pool) kwa ajili ya malengo hayo ambapo pesa hizo zinaweza zikazalishwa kwa faida ktk biashara ambazo ni halali kwa mtazamo wa maadili ya ki- Islam. Kama biashara hiyo itapata faida wanagawana faida hiyo, na kama itapata hasara basi pia wanagawana hasara hiyo. Ufafanuzi zaidi ktk tofauti zilizopo kati ya bima mbili hizi bado unahitajika.

kwa maelezo zaidi fuatilia maelezo yafuatayo:

 Tunapenda kuwafahamisha wafuatiliaji wetu kwamba ijue bank ya kiislam imebadilika kutoka kwenye blog na imekua website. Kufuatia mabadiliko hayo ijue bank ya kiislam kama blog itabaki kama ilivyo lakin hakutakua na taarifa zozote mpya badala yake wafuatiliaji wetu wanaombwa kutembelea www.ijuebenkyakiislam.com 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...