Wakati uchumi wa Tanzania ukiendelea kukua siku hadi siku, ongezeko la wananchi wenye kipato cha kati nalo limezidi kukua, na hivyo kuleta changamoto mpya katika masoko ya bidhaa mbalimbali hapa Waagizaji wa kinywaji Kutoka Uholanzi cha Bavaria eneo la Afrika ya Mashariki, Jovet (Tanzania) Limited wamedhamiria kuleta changamoto hiyo baada ya kuzindua kampeni rasmi ya mbio za kuelekea kileleni, na hivyo kuongeza wigo wake katika soko hili la Afrika ya Mashariki, ambalo limekua likikua kwa kasi kiuchumi.

Akiongea katika chakula cha jioni na mawakala wakubwa wa kinywaji hicho katika eneo la Afrika ya Mashariki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, bwana John Kessy, Mkurugenzi mkuu wa Jovet (Tanzania) Limited, alisema, Kampeni hii ya Bavaria ya kuelekea kileleni imelenga kuleta changamoto kubwa katika eneo hili la Afrika ya mashariki, kwa kuwa litasaidia kutengeneza ajira zaidi, na kuongeza kipato binafsi na kwa serikali kwa ujumla.

Bwana Kessy aliongeza na kusema kuwa, Tumeweza kupenya katika soko hili na kutengeneza mahusiano mazuri na wafanyabiashara. Tutaendelea kukua siku hadi siku tukiwapatia wateja wetu kilicho Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia hamsini ya wanywaji wa vinywaji vya shayiri wako eneo la Mashariki ya kati na Afrika na asilimia hii hutumia hektolita milioni 18 kwa mwaka, na hii imetokana na kwamba watu wengi wamekua wakijali zaidi afya zao, na hivyo Bavaria inataka kutumia fursa hii kujikita zaidi katika eneo hili, na kuwapa fursa walaji kupata uchaguzi zaidi.

Mawakala hawa pia waliweza kupata fursa ya kujifunza mengi kuhusu kinywaji cha Bavaria, na pia mbinu za kufanya biashara katika siko hili ambalo limekua likikua kwa kasi na lenye ushindani mkubwa. Pamoja na kujifunza mengi kuhusu Bavaria na mbinu za kibiashara, mawakala hao pia waliweza kujishindia zawadi mbalimbali, zikiwemo seti za Televisheni, Simu za Mkononi na vinywaji mbalimbali vya familia ya Takwimu za hivi karibuni za mwaka 2010-2015 zinaonyesha kuwa soko la vinywaji linatarajiwa kukua na kuzalisha zaidi ya dola za kimarekani bilioni 1.9, na tafiti hii
Mkurugenzi Mkuu wa Kovet (t) limited,Ndugu John Kessy akitafakari jambo wakati wa uzinduzi wa kampeni yam bio za kuelekea juu na Bavaria zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Jovet (t) Limited Ndugu John Kessy akimpongeza Bi. Christina wa K-Pub, kama mmoja wa mawakala bora wa kinywaji hicho.
Mkurugenzi wa Jovet,Ndugu John Kessy akifurahi jambo na wakala kutoka Rwanda Ndugu Innocent Gasangwa.
Baadhi mawakala wa Bavaria wakibadilishana mawazo wakati wa chakula cha jioni katika hoteli ya serana, Jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...