Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akizungumza na Maaskofu wa Kanisa la Moravian nchini baada ya kuwasikiliza malalamiko yao kuhusiana na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea kwa muda mrefu katika Kanisa hilo. Maaskofu hao ambao walikuwa wanaongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Alinikisa Cheyo walimuomba Waziri Chikawe aingilie kati kwa kudhibiti vurugu hizo ambazo zinazisambaratisha kanisa lao. Hata hivyo, Waziri Chikawe aliahidi kulifanyia kazi suala hilo na atalitolea maamuzi baada ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kukutana na pande zote mbili zinazogombana.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Askofu wa Kanisa la Moravian nchini, Conrad Nguvumali (watatu kulia) wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Chikawe jijini Dar es Salaam leo. Maaskofu watano wa Kanisa hilo ambalo limekumbwa na mgogoro kwa muda mrefu sasa, wakiongozwa na Askofu Kiongozi wa Kanisa hilo nchini, Alinikisa Cheyo (wapili kushoto) walionana na Waziri huyo ili kuomba msaada wake katika kudhibiti vurugu zinazoendelea katika Kanisa hilo. Hata hivyo, Waziri Chikawe aliahidi kulifanyia kazi na hatimaye kulitolea maamuzi suala hilo baada ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kukutana na pande zote mbili zinazogombana. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kwa kweli Bwana yesu awasamehe badala ya kumuambia roho mtakatifu aingilie kati kuleta amani ndani ya kanisa mnamuambia binadamu aingilie kati. Huduma hiyo mmeitwa na Mungu kweli hata kukosa ufahamu huo wa kutambua nani asululishe?

    ReplyDelete
  2. Wafanyabiashara hao hawana roho mtakatifu, Watu wa Mungu hawawezi kugombana mbele ya nyumba ya bwana.

    ReplyDelete
  3. hata mimi nilipoona ili nikawaza siasa za nini kanisani?
    kwanini wenyewe viongozi na waumini mnashindwa kujadiliana na kupata ufumbuzi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...