Ndugu Joseph Makani, Mkurugenzi Mifumo ya Komputa akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA, wakati wa uzinduzi wa kuanza kwa zoezi la Usajili na Utambuzi wa Watu mkoani Mtwara.
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imezindua rasmi zoezi la Usajili na Utambuzi wa Watu kwa wananchi na wakazi wa mkoa wa Mtwara, zoezi ambalo litadumu kwa siku 14 kuanzia Jumatatu tarehe 18/08/2014.
 Akizungumza katika sherehe fupi ya uzinduzi wa zoezi hilo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho; ndugu Joseph Makani amesema kuanza kwa zoezi hilo Mtwara ni utekelezaji wa mpango wa Usajili wa wananchi na wakazi waishio kihalali nchini wenye lengo la kuwapatia vitambulisho vya Taifa Raia, Wageni na Wakimbizi baada ya zoezi kama hilo kukamilika wa wananchi wa Tanzania Zanzibar, mikoa ya Dar-es-salaam, Pwani na sasa Mtwara.
Amesema ufanisi wa zoezi hilo unategemea sana ushirikiano toka kwa viongozi katika serikali, vyama vya siasa na viongozi wa Dini ambao walikuwepo kushuhudia tukio hili. 
Naye mgeni rasmi kaimu Katibu Tawala Mkoa ndugu Jehasen Bukwali kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ameahidi kutoa ushirikiano na kusimamia kwa dhati zoezi hilo kufanyika katika mkoa wa Mtwara, huku akiwataka viongozi katika ngazi zote kushiriki kikamilifu katika kufanikisha zoezi la Usajili ambalo linamatokea makubwa katika ustawi na maendeleo ya Taifa.
Amewaasa wananchi na wanasiasa kutohusisha zoezi hilo la Siasa, kwani vitambulisho vya taifa havihusiani na itikadi za chama chochote, na haki ya kila Mtanzania kusajiliwa na kupata haki yake msingi kikatiba.

Ufunguzi huo uliwakilishwa na viongozi katika ngazi za juu Mkoa, na Wilaya zikiwemo kamati za Ulinzi na Usalama. (picha na Rose Mdami (NIDA) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...