Pikipiki aina ya Suzuki ikiwa imenasa mbele ya Lori baada ya kugongana uso kwa uso .
Baada ya ajali hiyo pikipiki ilibaki ikiwa imesimama baada ya kunasa chini ya Lori la mafuta.
Askari wa kikosi cha usalama barabarani wakiwa katika eneo la tukio kwa ajili ya kufanya vipimo.
Na Dixon Busagaga wa Globu
 ya Jamii kanda ya Kaskazini.


Ajali mbaya imetokea barabara kuu ya Arusha Moshi ikihusisha Lori aina ya Sacania lenye namba za Usajili T 137 ATA na pikipiki aina ya Suzuki yenye namba SU 40262 mali ya Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA).



Mashuhuda wa ajali hiyo waliiamia Globu ya Jamii kuwa ilitokea majira ya saa 7 katika makutano ya barabara ya Arusha/Moshi na ile itokayo chuo cha polisi Moshi kuelekea ofisi za mkuu wa wilaya ya Moshi.



Katika ajali hiyo mwndesha pikipiki aliyefahamika kwa jina la George Lyamuya, mfanyakazi wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi, alifariki dunia papo hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...