Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe
(wapili kulia) akimshukuru Ofisa wa Mawasiliano na Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom
Tanzania, Georgia Mutagahywa (kushoto) baada ya kupokea hundi yenye thamani ya
Sh. Milioni 40 msaada uliotolewa kwa ajili ya Wiki ya Nenda kwa Usalama
Barabarani inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu,
jijini Arusha. Wapili kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest
Mangu, na kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna,
Mohamed Mpinga.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe
(wapili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya
kupokea hundi ya Sh. Milioni kwa ajili
ya maandalizi ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, kutoka kwa Ofisa wa
Mawasiliano na Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa
(watatu kulia). . Picha zote na Felix
Mwagara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani inatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, jijini Arusha. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Wapili kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, na kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo.
Picha zote na Felix Mwagara
wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...